
Mafikizolo wakiwasili Airport Dar leo
Baada tu ya kutua kwa ndege katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa JK Nyerere majira ya mchana eNewz ilihojiana na kundi zima la Mafikizolo, ambapo wamesema wamejipanga katika kutoa burudani kali hapo kesho litakalowaacha Watanzania na kumbukumbu isiyosahaulika.
Kazi inabaki moja tu, ni kwa wewe kudondoka pale Mlimani City siku ya kesho kuanzia majira ya saa moja usiku kwa ajili ya shoo kali ya Mafikizolo inayoletwa kwako na Juegga Cassa kwa udhamini wa nguvu wa East Africa Radio na East Africa Television.