
Madee
Madee amesema kuwa, huu unakuwa ni wakati muhimu kwake kama baba baada ya kupata rasmi haki ya malezi ya mwanae huyo yaani custody, baada ya kumaliza matatizo ambayo hakupenda kuyaweka wazi, hii ikiwa ni nafasi adhimu ya kukaa na mwanae mpaka atakaporudi shule mwezi Januari mwakani.
Baba Saida pia akatumia nafasi hii kutoa somo la malezi kwa wazazi wenzake, hususan ma-Single Daddies akigusia umuhimu wa kujenga urafiki na watoto wao, kutokana na mambo kubadilika na utandawazi kukuwa, akitaka mzazi kuwa na urafiki mkubwa na mwanae na kumtengenezea mazingira ya kuwa huru kuuliza mzazi chochote kile ambacho wanakumbana nacho, iwe kibaya ama kizuri kwa lengo la kujifunza.

