Sunday , 13th Jul , 2014

Baada ya taarifa kutoka kwa msanii Cindy wa Uganda kuelezea nia ya kufanya kolabo na kundi nyota la nchini Rwanda-Kigali, tayari kundi hilo limeweka taarifa wazi kwa mashabiki wao kuwa wamekubali kufanya nae kazi.

kundi la Urban Boys nchini Rwanda

Kundi hilo linalofanya miondoko ya Afro-Beat limekubali kufanya kolabo na Cindy baada ya mwanadada huyo kulifagilia kundi hilo baada kutumbuiza vyema hivi karibuni katika sherehe za siku ya ukombozi zilizofanyika hivi karibuni nchini Rwanda.

Mmoja wa memba wa kundi hilo Humble Gizzo ameelezea kuwa wanashukuru kupata sapoti yake kwani kufanya nae kazi itawasaidia kuukuza muziki wao zaidi ndani ya nchi za Afrika Mashariki.