Friday , 12th Jun , 2015

Staa wa muziki wa nchini Uganda, Edrisa Musuuza maarufu zaidi kama Eddy Kenzo ameamua kuongeza jina lake ambapo kuanzia sasa atakuwa akijulikana kama Eddy Kenzo Dada.

msanii wa muziki wa nchini Uganda Eddy Kenzo Dada

Marekebisho haya katika jina la staa huyo kwa mujibu wa taarifa yamechangiwa na moja ya shabiki wa staa huyo anayeishi huko Marekani, ambaye alielezwa na rafiki zake kuwa kitu cha pekee walichokifahamu kuhusu Uganda kabla ya msanii huyo ni Historia ya aliyekuwa dikteta wa nchi hiyo, Marehemu Idd Amin Dada.

Kwa sasa staa huyo anajivunia nafasi kubwa ya kutangaza nchi yake nje ya mipaka akiwa na rekodi ya kusafiri nchi mbalimbali ndani na nje ya bara la Afrika kutumbuiza.