Thursday , 20th Nov , 2014

Hatimaye mwanamuziki wa kike maarufu nchini Uganda Desire Luzinda, ameongea na maafisa upelelezi wa polisi kuhusiana na kusambaa kwa picha zake za utupu mitandaoni.

mwimbaji wa nchini Uganda Desire Luzinda

Luzinda alifika makao makuu ya polisi juzi usiku na kwenda moja kwa moja katika ofisi ya msemaji wa polisi ambapo alihojiwa na wapelelezi kwa muda wa saa mbili.

Vyanzo vya polisi vimesema Luzinda ametoa maelezo yanayomtuhumu aliyekuwa mpenzi wake kwa kuvujisha picha hizo kwenye mitandao ya jamii.