Wednesday , 1st Feb , 2017

Msanii wa bongo fleva Dayna Nyange amewasihi wasanii wa kike nchini kujifunza kuandika nyimbo zao wenyewe ili kuweza kupata 'melodi' na mizuka ya kuimba nyimbo nzuri.

Dayna Nyange

Akipiga story ndani ya eNewz  ya EATV amesema "siyo vibaya kuandikiwa wimbo lakini kwa wakati mwingine ni vizuri kujua kujiandikia mwenyewe kwani unaweza kupata zali la kuingia studio kubwa hata nje ya nchi na kupata nafasi ya kurekodi hata na wasanii wakubwa ukashindwa na ukapoteza zali kwa kuwa hujui kuandika".

Pia Dayna hakusita kumwagia sifa msanii mwenzake Maua Sama kwani anadai aliwahi kusikia kuwa ni mmoja kati ya wasanii wa kike wanaoweza kujiandikia nyimbo na kumsifia kwamba ni mwandishi mzuri.