Baadhi ya familia zilizokosa makazi nchini Syria
Mkuu wa misaada ya kibinadamu wa umoja wa mataifa Stephen O'Brien amesema maelfu ya watu wengine wanatarajiwa kuukimbia mji huo kutokana na mapigano yanayoendelea na kuimarika katika siku zijazo.
O'Brien ameonesha wasiwasi kuhusu hatma ya raia hao wanaoyakimbia mapigano na kuainisha kuwa yanatia shaka.majeshi na wapiganaji wa jeshi la Syria wamekamata theluthi mbili ya mji uliokuwa ukishikiliwa na waasi Mashariki ya Aleppo tangu mwishoni mwa juma.





