Tuesday , 8th Apr , 2014

Wakazi wa jiji la Dar es Salaam nchini Tanzania wamesema ujenzi wa barabara usiozingatia kuwepo kwa mifereji ya kupitishia maji ni moja ya sababu inayochangia barabara nyingi za jiji kushindwa kupitika wakati wa mvua.

Athari za mvua jijini Dar es Salaam

Wakizungumza na EATV mara baada ya kushuhudia barabara kadhaa zikiwa hazipitiki baada ya mvua kunyesha na kutuama maji wakazi hao wa jiji wamezitaka halmashauri za jiji kuzingatia ujenzi wa mifereji wanapoingia mikataba na wakandarasi wa kujenga barabara.

Wamesema tatizo hilo limekuwa ni endelevu hata kwa barabara zinazojengwa jambo ambalo wamesema lisiposimamiwa vema kila mwaka mvua zinaponyesha barabara zitakuwa zikijaa maji na kukosa suluhisho la kudumu.