
Kaimu mkuu wa wilaya ya Morogoro Bi. Betty Mkwasa
Wakizungumza baada ya kuapishwa kwa baraza jipya la halmashauri ya wilaya ya Morogoro, wananchi hao wamewataka viongozi waliowachagua kuhakiksha wanatilia mkazo suala zima la maendeleo ikiwemo utekelezaji wa miradi na huduma za kijamii ikiwemo maji, zahanatii, barabara na elimu bora na changamoto ya rushwa.
Kaimu mkuu wa wilaya ya Morogoro Bi. Betty Mkwasa amewataka madiwani kushirikiana na wananchi kuhakikisha wanakomesha migogoro ya wakulima na wafugaji, huku mkuu wa mkoa wa Morogoro Dkt.Rajab Rutengwe akisisitiza viongozi wanaochaguliwa kulinda amani ya nchi kwa gharama yeyote
Halmashauri ya wilaya ya Morogoro imemchagua kwa mara nyingine bi Kibena Kingo kuwa mwenyekiti mpya wa baraza hilo la madiwani.