Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Uhaba wa waalimu wakosesha wanafunzi masomo

Sunday , 23rd Apr , 2017

Shule ya Msingi Kitumbi iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma inakabiliwa na uhaba mkubwa wa walimu, ikiwa na wakufunzi wanne kwa ajili ya wanafunzi zaidi ya 300 hali inayosababisha wanafunzi kukosa masomo stahiki.

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Kitumbi, Igno Ndunguru ameyasema hayo hivi karibuni kuwa shule yake ina wanafunzi 335 lakini ina walimu wanne tu huku mmoja akiwa ni mgonjwa wa muda mrefu.

Nduguru amefafanua tatizo hilo la upungufu wa walimu lipo kwa muda mrefu, hali ambayo inapelekea kushindwa kufundisha wanafunzi hao masomo yote na kwa vipindi  husika kwa madarasa yote kama ilivyopangwa na wizara ya elimu.

Aidha amefafanua kuwa tayari uongozi wa wilaya ulipewa taarifa ya tatizo hilo na kwamba Serikali imesema italitatua itakapoanza kutoa ajira kwa walimu wapya.

 Kwa upande wa Diwani wa Kata ya Kipapa, Essau Ndunguru naye amekiri  na kudai kuwa ni kero yake ya muda mrefu ambayo kila mara kwenye baraza la madiwani huiwasilisha na kudai kuwa mbali na Kitumbi, tatizo kama hilo lipo pia katika Shule ya Msingi Kihongo.

“Naiomba sana Serikali ione umuhimu wa kuwaleta walimu ili waweze kukabiliana na uhaba katika shule za msingi za kata ya Kipapa kwani mazingira ya utolewaji wa elimu bora kwa wanafunzi ni mbovu sana," alisema Diwani  Ndunguru.

Afisa Elimu wa Shule za Msingi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, Samwel Komba alisema kuwa kwa ujumla halmashauri hiyo ina kabiliwa na tatizo kubwa la walimu kwani idadi ya walimu waliopo ni ndogo sana na kwamba mahitaji ya walimu ni makubwa ambapo kwa mfano shule ya Msingi Kihongo ina wanafunzi zaidi ya 600 lakini ina walimu watano.

 

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine