Wednesday , 9th Nov , 2016

Wizara ya Kilimo, Mifugaji na Uvuvi inatarajia kusambaza zaidi ya tani 32,300 za  mbolea ya kupandia  mazao zenye thamani ya shilingi billioni 30 kwenye mikoa 25 ili kuwawezesha wakulima kulima kilimo chenye tija na kuweza kupambana na baa la njaa.

Dkt. Charles Tizeba

 

Akizungumza na Waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam leo katika Ghala Kuu la Mbolea,  Meneja wa Kampuni ya serikali ya kuzalisha mbolea  nchini-TFC,  Salum Mkumba amesema kuwa katika wiki mbili zijazo maeneo yote yaliyopangiwa na wizara kupata mbolea hiyo ambayo ni ya ruzuku yatakuwa yameshapata mbolea hizo ambazo zitapekelewa kwenye uongozi wa kijiji kwa ajili ya kuwagawia wahusika.

Amebainisha kuwa mpaka sasa zoezi la usambazaji wa mbolea hizo limeshaanza hivyo amewataka wakulima wote nchini kujiandaa kuzipokea kwa ajili ya kurutubisha mimiea yao ambapo kwa siku wanatarajia kusambaza Tani 700 hadi 900 kwa siku.

Naye  Mkurugenzi Msaidizi sehemu ya Pembejeo kutoka Wizara ya Kilimo, Miguo na Ufugaji  Shenali  Nyoni ameeleza kuwa mbolea hiyo itapelekwa hasa kwenye maeneo yanayozalisha mazao ya mahindi na mpunga kwa kiasi kikubwa hasa mikoa ya nyanda za juu kusini.