Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Sumaye aweka wazi kuhusu kurudi CCM

Tuesday , 22nd Aug , 2017

Waziri Mkuu Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Tatu, Frederick Sumaye amesema kunyang'anywa mashamba yake si sababu ya yeye kufikiria kurudi CCM kwani wakati anaondoka na kuhamia CHADEMA aliamua kwa hiari yake mwenyewe kwa kuzingatia maslahi ya umma.

Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye

Akizungumza leo na Wanahabari, Mhe. Sumaye ambaye pia sasa ni Mwenyekiti wa CHADEMA kanda ya pwani amesema kwamba tangu kuondoka ndani ya Chama cha Mapinduzi amekuwa akiandamwa kwa na maneno pia na visa mbalimbali vya kumkatisha tamaa ya kuendelea kubaki upinzani lakini haiwezi kuwa rahisi yeye kubadilisha msimamo aliouweka.

“Kunyang’anywa mashamba yangu najua ni uamuzi wa juu haunidhoofishi nifikirie kurudi CCM. Suala la kufikiri kuninyang'anya mashamba itakuwa sababu ya kunirudisha CCM ni ndoto ya mchana, nilihama kwa maslahi ya wananchi na nilishasema mbele ya wanahabari kitakachonifanya nirudi CCM ni mpaka CCM itoke madarakani. lakini sina haja ya kurudi ,’’ Sumaye

"Wanataka nirudi CCM, mimi sitaki kurudi CCM, kwanini wananilazimisha? Nilisema sababu za kuondoka huko, waseme wazi sababu za kuyafuta mashamba yangu ni za kisiasa tu," aliongeza

Akizungumza kuhusiana na mashamba yake yaliyochukuliwa na Serikali, Mh. Sumaye amesema anashangaa kuambiwa kwamba mashamba yake hayalipiwi kodi wala kuendelezwa wakati shughuli nyingi zikiwemo ufugaji na kilimo zinafanyika ikiwa ni pamoja na umiliki wa kisheria.

Pamoja na hayo Sumaye amewataka viongozi waliopo madarakani kutotumia visasi vya kisiasa kumfilisi kwani chama cha upinzani kipo kisheria na pia siyo dhambi.

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine