Rais Magufuli alipotembelea bandarini na kukutana na mchanga wa dhahabu uliokuwa tayari kusafirishwa nje ya nchi
Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa kamati hiyo yenye wajumbe 8, inatakiwa kuanza kazi haraka iwezekanavyo.
Wajumbe wa Kamati hiyo ni;
- Prof. Abdulrahman Hamis Mruma
- Prof. Justianian Rwezaura Ikingula
- Prof. Joseph Bushweshaiga
- Dkt. Yusuf Ngenya
- Dkt. Joseph Yoweza Philip
- Dkt. Ambrose Itika
- Mohamed Zengo Makongoro
- Hery Issa Gombela
Wajumbe wote wa kamati hii wanatakiwa kufika ofisi ya Katibu Mkuu Kiongozi, Ikulu Jijini Dar es Salaam Ijumaa tarehe 31 Machi, 2017 saa 4:00 asubuhi.