Monday , 13th Jun , 2016

Aliyekuwa mwenyekiti wa CUF Prof. Ibrahim Haruna Lipumba amemuandikia barua Katibu Mkuu wa Chama hicho Maalim Seif Sharif Hamadi ya kuomba kutengua barua yake ya mwaka yana ya kujiuzulu nafasi yake ya uenyekiti wa chama hicho.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam Prof Lipumba amesema kwamba ameandika barua hiyo na anasubiri uamuzi wa chama hicho kama utaamua kumrejesha au la.

Hatua ya Lipumba inatokana na Chama cha CUF kutangaza uchaguzi wa kuziba nafasi zilizo wazi katika chama hicho ikiwemo nafasi ya uenyekiti iliyokuwa iliyokuwa wazi baada ya kujiuzulu kwa lipumba.