Friday , 8th Jul , 2016

Maafisa polisi wanne wa Dallas nchini Marekani wamepigwa risasi na kufa na wengine saba kujeruhiwa, wakati wa maandamano ya kupinga vitendo vya polisi kuwapiga risasi na kuwauwa watu weusi.

Mmoja wa watuhumiwa anashikiliwa na polisi baada ya kutupiana risasi na polisi, huku mtu mmoja mwingine akijisalimisha polisi, kwa mujibu wa twitti ya polisi.

Milio ya risasi ilisikika wakati waandamanaji hao wakiandamana Mjini Dallas, katika maandamano yaliyochochewa na vifo vya Philando Castile huko Minnesota na Alton Sterling huko Louisiana, waliouwawa na polisi kwa risasi.