Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Norway yaipa angalizo Tanzania

Tuesday , 19th Jun , 2018

Serikali ya Tanzania imepewa angalizo na Norway ya kuweka mifumo thabiti ya uwekezaji wenye faida ukiwemo ule wa sekta ya madini, kukamilika mapema ili kuweza kutoa fursa kwa wawekezaji wapya kuwekeza kwenye sekta hiyo kwa wakati.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Shirika la Maendeleo la Norway (NORAD), Bw. Jon Lamoy wakati alipokuwa anazungumza na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga ambaye yupo nchini humo kwa ziara yake ya kikazi ya siku tatu Mjini Oslo makao makuu ya Norway.

"Jitihada za Tanzania za kupambana na rushwa, hususan kwenye ukusanyaji kodi, zitawawezesha wananchi wa Tanzania kunufaika na huduma za kijamii na hatimaye kupata maendeleo kwa haraka. Ni muhimu mkakamilisha mapema mifumo thabiti ya uwekezaji wenye faida ili kutoa fursa kwa wawekezaji wapya kuwekeza kwenye sekta ya madini kwa wakati", amesema Mkurugenzi Lamoy.

Kwa upande wake, Dkt. Mahiga amedai kuwa suala hilo tayari linafanyiwa kazi ambapo pamoja na serikali kuweka mazingira rafiki kwa wawekezaji, uwekezaji huo ni lazima uwe na faida kwa watanzania na kwa maendeleo ya nchi.

"Serikali ya Rais Magufuli imedhamiria kuipeleka Tanzania kwenye uchumi wa kati unaoongozwa na sekta ya viwanda. Katika kutekeleza hilo, serikali imepitia na kurekebisha baadhi ya sheria na mikataba ambayo ilikua inanufaisha upande mmoja", amesisitiza Dkt. Mahiga.

Kwa upande mwingine, Dkt. Mahiga amesema marekebisho yanayofanyika sasa yanalenga kwenye kuleta faida kwa pande zote mbili yaani 'win win situation'.

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine