Tuesday , 7th Jun , 2016

Waislam nchini Tanzania wametakiwa kuutumia mwezi Mtukufu wa Ramadhani, ulioanza hii leo kwa kuwasaidia watu mbalimbali ikiwemo wenywe mahitaji maalumu na kufanya ibada ili wapate baraka kutoka kwa mwenyezi Mungu.

Kiongozi Mkuu wa dini ya kiislam wa madhebu ya Shia, ithana Sharia, Sheikh Hemed Jalala

Wito huo umetolewa na Kiongozi Mkuu wa dini ya kiislam wa madhebu ya Shia, ithana Sharia, Sheikh Hemed Jalala wakati akiongea na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam alipozungumzia mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Sheikh Hemed pia amesema waislam waendelee kutumia mwezi mtukufu wa Ramadhani kwa kudumisha amani na utulivu nchini lakini uwe mwanzo wa mabadiliko ya amani ya kweli kwa maendeleo ya taifa la Tanzania

Aidha Sheikh Hemed pia amaetumia fursa hiyo kulaani vikali vitendo vya mauaji ya waumini wa kiislam kwenye nyumba ya ibada Jijini Mwanza pamoja na watu nane waliouwa mkoani Tanga na kusema kuwa jambo hilo kamwe halikakubali kwenye Ardhi ya Tanzania yenye amani

Kiongozi Mkuu wa dini ya kiislam wa madhebu ya Shia, ithana Sharia, Sheikh Hemed Jalala