Licha ya pesa hizo kuwa tayari zimetolewa na wafadhili, mpaka sasa ni shule moja pekee yenye uhakika wa kukamilika kwa asilimia 99.
Mkurugenzi wa Wilaya ya Kilombero, Dennis Londo amesema kuwa miradi hiyo ambayo inafadhiliwa na Benki ya Dunia inatakiwa kukamilika Desemba 30 mwaka huu, lakini amewatupia lawama wakandarasi ambao wamepewa tenda hiyo kutokamilisha kwa wakati.
Kutokana na hali hiyo Mkurugenzi huyo amesema kuwa endapo fedha hizo hazitatumika kwa muda uliopangwa fedha hizo zitarudishwa kwa mfadhili kitendo ambacho kitaisababishia serikali hasara kuanza kujenga miradi hiyo, wakati pesa zote zimeshatolewa na Benki ya Dunia.
Hata hivyo amesema kuwa serikali imeamua kufuatilia ujenzi wa miradi hiyo kuhakikisha kuwa kabla ya desemba 30 mwaka huu iwe imekamilika, ili wananchi wapate huduma ambayo inastahili.
Sikiliza hapa majibizano kati ya mkurugenzi na wakandarasi............