Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mikoa yote yatakiwa kuwa na huduma ya methadone

Tuesday , 21st Feb , 2017

Serikali imeagiza hospitali zote za mikoa nchini zianzishe kliniki maalum ya kutoa huduma za matibabu ya watumiaji wa dawa za kulevya kwa kutumia methadone, ndani ya miezi sita.

Dkt Kigwangalla katika ziara yake, Mwananyamala

 

Agizo hilo limetolewa na Naibu wa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla alipotembelea kituo cha kuwahudumia watu wanaotibiwa kuacha dawa za kulevya kwa kutumia methadone kilichopo Hospitali ya Mwananyamala na kumuagiza Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya kuhakikisha kuwa kuna Daktari Bingwa wa Afya ya Akili kwenye kila mkoa ili kuanzisha na kusimamia vituo hivyo.

Dkt. Kigwangalla amesema kumekuwepo na ongezeko kubwa la watu wanaohitaji huduma hiyo kwa siku za hivi karibuni kutokana na kuongezeka kwa udhibiti wa dawa za kulevya, huku kukiwapo kwa taarifa kwamba wauzaji wa dawa za kulevya wameathiriwa kwa kupoteza mapato ya shilingi bilioni 70.

Pamoja na mambo mengine Dkt. Kigwangalla amekemea baadhi ya viongozi wanaopotosha jamii kuhusu dawa hizo methadone.

Kwa upande wake muangalizi wa kituo hicho Dkt. Kasian Ndindindi amesema uwepo wa kituo hicho cha Mwananyamala kwa sasa umesaidia kuwahudumia waathirika wa dawa za kulevya 3,351.

Nao baadhi ya watu wanaopatiwa huduma katika kituo hicho wamesema tangu waanze kutumia dawa hizo wamekuwa na unafuu mkubwa

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine