Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kitila Mkumbo aanika ukweli

Thursday , 12th Oct , 2017

Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na umwagiliaji Profesa Kitila Mkumbo, ameweka wazi sababu ya yeye kukubali kuteuliwa kushika wadhifa huo, licha ya misimamo ambayo alikuwa nayo awali, dhidi ya wasomi wanaoteuliwa kushika wadhifa mkubwa serikalini.

Akizungumza kwenye kipindi cha East Africa Breakfast kinachorushwa na East Africa Radio, Prof. Mkumbo amesema kilichofanyika kwake ni kupandishwa cheo kutoka nafasi aliyokuwa nayo awali, na asingeweza kukataa kwani ni heshima kubwa aliyopewa na Rais.

“Wakati nimeteuliwa na Rais, mimi nilikuwa mtumishi wa umma, nilipandishwa cheo kutoka chuuo kikuu mpaka ukatibu mkuu, nani huyo akipandishwa cheo atakataa!!? Mimi nilikuwa mtumishi wa umma, hiyo ni heshima kubwa niliyopewa”, amesema Kitila Mkumbo

Prof. Mkumbo ameendelea kwa kusema kwamba baada ya kuteuliwa huko hakuchelewa kuachia wadhifa ambao alikuwa nao kwenye chama cha ACT- Wazalendo, kwa kuwa aliona dhahiri asingeweza kuendeleza harakati alizokuwa anafanya kwenye chama.

“Katika nafasi ya Katibu mkuu, mimi sio tu mtumishi wa umma, mimi ni serikali nawajibika kwa serikali kuisimamia, kutekeleza mipango ya serikali, tofauti kabisa na uhadhiri, kwenye chama nilikuwa nafanya harakati, nikaona hili sasa haliwezekani, ikabidi niwaombe wenzangu kwamba hapa nilipofika majukumu haya siwezi kuchanganya na uanachama wangu, ikabidi niweke uanachama pembeni”, amesema Kitila Mkumbo.

Hivi karibuni Kitila Mkumbo amejiondoa unachama wa ACT- Wazalendo, akisema kwamba hatoweza kutumikia serikali akiwa mwananchama wa chama hicho, kwani kuna mgongano wa maslahi.

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine