Wednesday , 28th Nov , 2018

Viongozi mbalimbali wa vyama vya upinzani nchini akiwemo Kiongozi wa Chama cha ACT – Wazalendo, Zitto Kabwe na Naibu Katibu Mkuu wa CUF bara upande wa Maalim Seif , Joel Luhabara wameonekana kwenye kesi ya dhamana inayomkabili Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA,

Freeman Mbowe pamoja na Mbunge Ester Matiko.

Mbali na viongozi hao wakubwa pia mahakamani hapo ilishuhudiwa mamia ya wafuasi wa CHADEMA waliojitokeza kwaajili ya kusikiliza hatma ya kiongozi wao Freeman Mbowe.

Tunawaambia wanachama wote kesho saa mbili waje mahakamani, chama chote kitahamia hapa, naomba wanachadema tushikamane kwa ajili ya mwenyekiti wetu.” Amesema Borniface Jacob

Akizungumza nje ya viunga vya mahakama Naibu Katibu Mkuu CUF bara Joel Luhabrua amesema “kwa hali ilivyosasa kuna nguvu ya kutaka kuumiza upinzani, tumeona tuongeze nguvu yetu kwa pamoja, ” Joel Luhabura

Mbowe na Matiko wamerudishwa rumande kwaajili ya kusubiri kusikilizwa kwa kesi ya kupewa au kutopewa dhamana, Alhamisi ya wiki hii saa mbili asubuhi.