Saturday , 18th Jun , 2016

Chama cha Mapinduzi kinatarajia kufanya mkutano wake mkuu maalumu tarehe 23 Julai mwaka 2016 wenye lengo la kubadilishana kijiti cha nafasi ya uenyekiti wa chama cha mapinduzi.

Katika taarifa iliyotolewa na Msemaji wa CCM Christopher Olesendeka imesema kuwa uamuzi huou mefikiwa baada ya kikao cha kamati kuu kukaa leo jijini Dar es salaam na kujiridhisha kuwa maandalizi yote ya mkutano huo yamekamilika.

Katika mkutano huo wa June inatarajiwa Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi Dkt Jakaya Mrisho Kikwete atamkabidhi maqdaraka ya uenyekiti wa chama hiko Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Magufuli.