Akiongea katika ufunguzi wa mkutano mkuu wa tatu wa bodi ya usajili wa wataalam wa mipango miji katibu mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Yamungu Kayandabila amesema tabia ya wataalamu hao inaipotezea serikali mapato ya kodi ya ardhi.
Dkt Yamungu amesema kuwa mbali na kuwachukulia hatua wataalam hao pia ameitaka bodi hiyo kuhakikisha inakomesha vitendo vinavyofanywa na baadhi ya taasisi za umma zikiwemo halmashauri na sekta binafsi wanatumia makampuni yasiyosajiliwa kupima ardhi.
Naye Mwenyekiti wa bodi ya usajili wa wataalam wa mipango miji Profesa Wilbard Kombe amesema kuwa mpaka sasa bodi imeanza kuhamasisha wananchi kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za upangaji miji ili kuepuka ujenzi holela na migogoro ya ardhi.

