Bi Khaleda ambaye ni Waziri Mkuu wa zamani amekana tuhuma za kutumia vibaya fedha za misaada ya kimataifa zilizotolewa kwa ajili ya kusaidia vituo vya watoto yatima nchini humo.
Kufuatia hukumu hiyo kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 72, hawezi kugombea katika uchaguzi wa Bunge utakaofanyika baada ye mwaka huu .
Hiyo ni moja ya mlolongo wa kesi zinazomkabili Bi. Khaleda ambaye ni mpinzani wa muda mrefu wa Waziri Mkuu wa sasa Sheikh Hasina .
Kiongozi huyo anatuhumiwa kutumia vibaya Dola 252,000 zilizotolewa kwa ajili ya watoto yatima .
Bi Khaleda alikuwa Waziri Mkuu wa Kwanza mwanamke mwaka 1991 akiongoza chama cha Bangladesh Nationalist Party, BNP.

