Wawepo wasaidizi wa sheria kwa vijana - Sengu LHRC
Serikali ijayo imetakiwa kuweka sheria ambayo itamfanya kijana kuwa na wasaidizi wa kisheria, ili kuweza kumsaidia kijana pale anapokuwa na uhitaji.
Rai hiyo imetolewa na Mwanasheria Hussein Sengu kutoka kituo cha msaada wa kisheria (LHRC), alipokuwa akiongea kwenye kipindi cha Super Mix kinachorushwa na East Africa Radio.
Sengu amesema kwamba asilimia kubwa ya watu wanaoingia katika migogoro ya kisheria ni vijana kutokana na kutokuwa na ajira na kutokuwa na matumaini ya kesho.