Spika Ndugai atangaza mabadiliko kwa Wabunge
Spika wa Bunge la Tanzania Job Ndugai, amesema Bunge hilo lina mpango wa kuacha kutumia mfumo wa sasa wa makaratasi Bungeni, kwa ajili ya kuwapa Wabunge nyaraka mbalimbali, watakachofanya sasa ni kuhamia katika mfumo wa Digitali, kwa kuwawekea kupitia kwenye simu zao.