''Makanisa yawe gereji'' - Goodluck Gozbert
Muimbaji wa nyimbo za Injili nchini Goodluck Gozbert amesema kuwa, Nyumba za Ibada hazipaswi kuwa kama Ofisi za Serikali, badala yake ziwe kama Gereji ambazo zitakuwa tayari kumpokea mtu wa aina yoyote ile na kumbadilisha kuweza kuishi maisha ya kumpendeza Mungu.