Ajifanya mtumwa kuhamasisha watu kujiandikisha
Katika hali isiyokuwa ya kawaida, kijana mmoja anayefahamika kwa jina la Ikuzi Kicheko (Mzalendo Halisi), ameshangaza watu kwa kuvaa mavazi yaliyokuwa yakivaliwa na watumwa enzi za ukoloni, huku akiwa amebeba bango linalohamasisha watu kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura.

