Lamine Yamal awatia hofu Barcelona

Lamine Yamal amewastua Viongozi pamoja na Mashabiki wa Barcelona kuelekea mchezo wa La Liga dhidi ya Mahasimu Wao Wakubwa Real Madrid (El Clasico). Nyota huyo mwenye umri wa miaka 17 alitolewa nje ya Uwanja akiwa anachechemea kwenye mchezo dhidi ya Denmark muendelezo wa mechi za mashindano ya Mataifa Ulaya.

Lamine Yamal amefunga goli 5 katika michezo 11 msimu huu ndani ya klabu yake ya Barcelona. Mchezo wa El Clasico unatarajiwa kuchezwa Oktoba 27, 2024 katika Uwanja wa Santiago Barnabeu . Yamal ametengeneza safu hatari ya ushambuliaji Barcelona akishirikiana na Robert Lewandoski, Rafinha.

Pages

Subscribe to East Africa Television RSS