Uzinduzi huo unaashiria dhamira ya serikali kupata majibu ya msingi kuhusu matukio yaliyotikisa amani ya nchi na kusababisha migogoro ya kisiasa.
Akitoa hotuba wakati wa uzinduzi wa Tume hiyo, Rais Samia alisisitiza wajibu mkuu wa Tume: kufukua mizizi ya matatizo. Alitaja maswali ya msingi ambayo Watanzania wanataka yajibiwe.
"Tume tunaitarajia ikatuangalizie, sababu hasa iliyoleta kadhia ile sababu hasa ni nini? Kiini cha tatizo ni nini?" - Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Tanzania.
