Ijumaa , 21st Feb , 2025

Pambano la bingwa wa dunia Daniel Dubois dhidi ya Joseph Parker siku ya Jumamosi halitakuwepo baada ya bingwa huyo kuugua siku mbili kabla ya pambano hilo.

Daniel Dubois - Bondia wa Nchini Uingereza

Muingereza huyo mwenye umri wa miaka 27 anayemiliki mkanda wa IBF  hapo jana alikosekana katika mkutano wa wanahabari  na baadaye akafanyiwa vipimo na kugundulika kuwa hatoweza kupambana katika pambano hilo

Kwa sasa Parker raia wa New Zealand mwenye umri wa miaka  33   atapambana na Mkongo Martin Bakole ambaye ameteuliwa kama mbadala wa Dubois anayeumwa .

Haijaelezwa bayana  ni nini hasa kinacho msibu Dubois ambaye alikuwa akipewa nafasi kubwa ya  kutetea taji lake la IBF kwa mara ya pili.