Leo Stars inakibarua cha kusaka pointi tatu dhidi ya DR Congo iliyotoka kugawana pointi mojamoja na timu ya taifa ya Morocco ambayo iliifunga Tanzania mabao 3-0 kwenye mchezo wa kwanza hatua ya makundi.
Ikiwa Stars itapata ushindi leo itafikisha pointi nne, kama Zambia itapoteza dhidi ya Morroco angalau kutakuwa na nafasi ya kutinga 16 bora ikishinda matumaini yatayeyuka.
Ipo wazi kuwa pointi moja waliyopata Tanzania ilikuwa kwenye mchezo dhidi ya Zambia walifunga bao la mapema dakika ya 11 kupitia kwa Simon Msuva katika dakika za lala salama Zambia iliweka usawa na kufanya ubao kusoma 1-1.