Yanga imepata ushindi wa magoli 2-0 dhidi ya Al-Merrikh ya Sudan ugenini ilhali Simba SC wao wametoka sare ya 2-2 dhidi ya Power Dynamos ugenini nchini Zambia. Yanga SC tayari imesharejea nchini ilhali Simba SC inataraji kurejea Jumatatu ya leo Septemba 18, 2023 kuanzia saa 8 mchana.
Wawili hao wamesema wataweka wazi harakati zao za maandalizi ya michezo yao ya marudiano huku kili timu ikionekana kujiamini kutokana na matokeo waliyoyapata kwenye mchezo wao wa kwanza.