Mahindi
Amos alipoteza maisha akiwa Zahanati ya Matui wakati akipatiwa matibabu kufuatia kipigo alichopata kutoka kwa wananchi
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kijiji cha Laalala Khalidi Soya Chubi, amesema awali mtuhumiwa huyo alikutwa na viroba vitatu vya mahindi ambayo hayajapukuchwa na kisha kupigwa na kundi la watu hao.
"Nilipata simu kutoka kwa mwananchi kuwa kuna mwananchi mmoja alionekana akiiba mahindi shambani na amezingirwa na watu, nikaenda huko ambapo niliwakuta na kuongozana naye mpaka kwa Mtendaji wa Kijiji na kuandikiwa barua kisha kwenda Zahanati ya Matui na huko alipofika akafariki," amesema Mwenyekiti