
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro, Juma Muhina
Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro, Juma Muhina, na kusema kwamba tayari serikali wilayani humo imeandaa utaratibu mzuri wa kufuta machozi kwa kila familia zilizofikwa na misiba ya watoto hao.
Siku ya tukio ilidaiwa kwamba watoto hao ambao walikuwa ni wanafunzi wa shule ya msingi Ngoile, walifikwa na mauti hayo mjira saa 4:00 usiku wakati wakitafuta mifugo yao iliyokuwa imepotea.
Serikali imeendelea kutoa wito kwa jamii za kifugaji zinazoishi karibu na hifadhi, kuchukua tahadhari kwa watoto pale wanapowapa majukumu ya kuchunga mifugo.