
Waziri wa Maji Jumaa Aweso
Waziri Aweso amefikia uamuzi huo wakati wa ziara ya kutembelea mradi wa kisima ambao upo katika Kijiji hicho baada ya malalamiko ya wananchi na hivyo kutoa maelekezo ya kusimamishwa kazi kwa Meneja huyo ambaye kwa sasa ni Meneja wilaya ya Hanang ambapo hapo awali mradi wa kisima cha maji Mkoka ulikuwa chini yake na uligharimu shilingi milioni 600.
Waziri Aweso amesema maabara ambayo imetumika kupima maji hayo imeonesha wazi kuwa maji hayo yana chumvi nyingi hivyo hayafai kwa matumizi ya binadamu.