
Gari na baadhi ya wachezaji wa Baobab Queens
Safari hiyo imekwama baada ya gari walilokuwa wakisafiria kushika moto kutokana na hitilafu za mfumo wa umeme kwenye gari.
Timu hiyo inaelekea mkoani Kigoma kwenye mchezo wa ligi kuu ya wanawake dhidi ya Kigoma Sisters utakaopigwa kesho.
Mpaka mchana huu wa Desemba 13, 2019, wachezaji wa timu hiyo na benchi la ufundi bado wapo Mabeshi ambapo mafundi wanaendelea kufanya marekebisho ili waweze kuendelea na safari.