Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Yanga yamtangaza mrithi wa Jerry Muro

Ijumaa , 14th Jul , 2017

Klabu ya Yanga kupitia Katibu Mkuu wake Charles Boniface Mkwasa leo wamemtangaza rasmi aliyekuwa Afisa habari wa Mbeya City Dismas Ten kuweza kuwatumikia wanayanga baada ya kuingia naye mkataba leo

Katibu Mkuu wa Yanga, Charles Boniface Mkwasa

Mkwasa amebainisha hayo kwenye mkutano wake na waandishi wa habari uliofanyika makao makuu ya klabu hiyo eneo la Jangwani Kariakoo Jijini Dar es Salaam ambapo Dismas anachukua nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Afisa Habari wa klabu hiyo Jerry Murro ambaye amemaliza kutumikia adhabu yake Julai 2 mwaka huu ya kutojihusisha na masuala ya mpira na Shirikisho la mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

"Tumeamua kuleta mapinduzi kwenye utoaji habari kwenye klabu yetu na naamini kwa muunganiko huu wa Dismas na Chicharito klabu yetu itafanikiwa sana kupitia kitengo hiki cha habari na mawasiliano kama vilabu vingine vikubwa duniani", amesema Mkwasa.

Pamoja na hayo, Mkwasa amesema nafasi hiyo ilikuwa ikikaimiwa na Godlisten Anderson Chicharito kama kaimu afisa habari ambaye sasa ataendelea na nafasi hiyo chini ya Dismas Ten.

                            Afisa habari mpya wa yanga Dismas Ten (katikati) akiwa anaongea 

Kwa upande mwingine, Mkwasa amedai mwenyekiti wa klabu hiyo bado anaendelea na zoezi la usajili na mambo yakiwa mazuri ataweza kuweka bayana ni mchezaji gani mpya wamemnasa.

 

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya