Mabingwa hao watetezi wa kombe la ligi ya soka Tanzania bara wataoneshana kazi na wapinzani wao majira ya saa 16:30 kwa saa za Tanzania sawa na saa 15:30 kwa saa za Mauritius.
Yanga watacheza leo mchezo huo kisha kukwea pipa na kutimkia kisiwani Zanzibar kwa ajili ya kambi ya kujifua kuwakabili watani zao wa jadi Simba SC katika mchezo wa marudiano wa ligi kuu utakaopigwa Februari 20 uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.
Kikosi cha Jangwani kinachotarajiwa kuanza kwenye mchezo huo wa ugenini kinaongozwa na wachezaji wafuatao;
1. Ally Mustafa ‘Barthez’
2. Juma Abdul
3. Oscar Joshua
4. Kelvin Yondan
5. Vicent Bosou
6. Thaban Kamusoko
7. Saimon Msuva
8. Haruna Niyonzima
9. Donald Ngoma
10. Amis Tambwe
11. Deus Kaseke
Watakaoanzia benchi ni pamoja na;
Deogratius Munishi ‘Dida’
Pato Ngonyani
Haji Mwinyi
Juma Said Makapu
Paul Nonga
Issoufou Boubakar Garba
Matheo Anthony





