Akizungumza na East Africa Radio Afisa Habari wa Azam FC Jaffar Idd Maganga amesema, wachezaji walioitwa na timu zao za Taifa ni Jean-Baptiste Mugiraneza ameitwa na timu yake ya Taifa ya Rwanda, Didier Kavumbagu akiwa na timu yake ya Taifa ya Burundi na Allan Wanga akiwa kaitwa na timu yake ya Taifa ya Kenya.
Maganga amesema, baadhi ya wachezaji wametolewa kwa mkopo kutokana kukosa nafasi hivyo wameenda kukuza vipaji vyao katika timu hizo.
Maganga amesema, licha ya wachezaji hao kuchukuliwa kwa mkopo na timu hizo lakini hawataweza kucheza mechi baina na Azam FC lakini Klabu hizo zimetakiwa kuwakatia wachezaji hao bima ya matibabu ambapo watatakiwa kutibiwa kama wachezaji wa Klabu kubwa.

