Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Spika apiga kijembe Yanga, Tarimba akipokea

Alhamisi , 8th Apr , 2021

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limeendelea leo Aprili 8, 2021, likiongozwa na Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai ambaye katika kipindi cha maswali na majibu alitupa kijembe kwa mbunge wa Kinondoni Abbas Tarimba kuhusu ushindi wa Simba SC.

Spika Job Ndugai na Mbunge Abbas Tarimba

Akimkaribisha kuuliza swali mbunge wa Kinondoni Spika Job Ndugai amesema kuwa Pasaka ya mwaka huu ilikuwa nzuri sana hasa baada ya ushindi wa Simba wa magoli 4-1 dhidi ya AS Vita kwenye uwanja wa Mkapa Dar es salaam.

“Niwaombe radhi waheshimiwa wabunge, lakini mtakubaliana nami Pasaka ya mwaka huu ilikuwa nzuri sana hasa baada ya mtu kupigwa bao 4-1, nashindwa kujizuia kumpa nafasi mbunge wa Kinondoni (Abbas Tarimba) asiulize swali,” amesema Spika Job Ndugai.

Aidha mbunge wa Kinondoni Abbas Tarimba naye akajibu kuwa amepokea kijembe hicho huku wakiwashauri Yanga SC kuitumia kama mfano ili kuendelea kuitangaza Tanzania kimataifa.

“Naona kijembe kimeingia sawasawa lakini na mimi ni wapongeze kwasababu Simba SC wameisaidia Tanzania kuweza kuonekana vizuri na ule utaratibu wa kuitangaza Tanzania “Visit Tanzania” kusema kweli ni jambo linalofaa kuigwa na wenzetu wa Yanga  pindi watapofanikiwa kuingia kwenye mashindano haya,” amesema Abbas Tarimba.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa