Jumanne , 29th Dec , 2015

Mabingwa wa Kombe la Mapinduzi Simba Sc wameomba mabadiliko ya Ratiba kwa waandaaji wa Michuano ya Kombe la Mapinduzi inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi Januari mbili Mwakani Visiwani Zanzibar.

Mkurugenzi wa mawasiliano wa Klabu ya Yanga Hajji Manara amesema wameomba waandaaji kuangalia ratiba yao kwani Januari Mosi wana mechi dhidi ya Ndanda Fc Mjini Mtwara huku wakiwa wamepangiwa kuanza Michuano ya Kombe la Mapinduzi Januari mbili mwaka huu.

Manara amesema, kama mabingwa watetezi wa michuano hiyo, Kikosi kimejipanga kwa ajili ya kushiriki michuano hiyo kwa kuweza kutetea kombe hilo.