![](http://eatv.tv/sites/default/files/styles/detailpageimg/public/news/2024/02/02/WhatsApp Image 2024-02-01 at 15.13.32.jpeg?itok=GcCFLQh1×tamp=1706870684)
Mahona amesema kuwa mafundi wanaendelea na kazi ya kutoa uchafu wote kwenye kuta za uwanja huo huku hatua inayofata ni uwekaji wa viti vipya ndani ya uwanja wa Mkapa.
’Tumeshaoneshwa mfano wa viti ambavyo vitawekwa na vipo kiwanda vinamaliziwa na hivi karibuni vitakuja Tanzania ‘’ amesema Mahona
Aidha Meneja Mahona ametoa raia kwa wanamichezo wanatumia uwanja huo kuwa wastarabu pindi wanapokuja kutazama timu zao.
Ikumbukwe kuwa mwaka jana 2023 Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo ilisaini Mkataba wa makubaliano ya ukarabati wa Uwanja wa Benjamin Mkapa na Kampuni ya Beijing Construction Engineering Group (BCEG) ya China ambao utagharamia zaidi ya Sh. Bilioni 31 na utarajiwa kukamilika Julai 2024.