Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Serena atwaa taji la Wimbledon kwa rekodi mpya

Jumamosi , 9th Jul , 2016

Mwanadada raia wa Marekani ambaye ni mchezaji bora namba moja kwa mchezo wa tenisi duniani kwa upande wa wanawake Serena Williams nyota yake imeendelea kung'ara tena katika michuano mikubwa ya tenisi ya Grand Slam akitwaa ubingwa wa Wimbledon.

Mwanadada Serena Willams akishangilia baada ya kushinda fainali ya Wimbledon.

Gwiji wa tenisi upande wa kinadada Serena Williams ameshinda fainali ya michuano ya ubingwa wa michuano mikubwa ya tenisi Grand Slam ya Wimbledon na kuifikia rekodi ya mchezaji Steffi Grafs ya kutwaa Grand Slam 22 kufuatia hii leo kufanikiwa kutwaa ubingwa wa Wimbledon baada ya kumduwaza Mjerumani Angelique Kelber kwa seti mbili mfululizo za michezo 7-5 na 6-3.

Serena mwenye umri wa miaka [34] ndiye aliyekua bingwa mtetezi wa michuano hiyo na sasa anaweka kibindoni taji la saba [7] la michuano hiyo mikubwa ya tenisi Wimbledon kwa kalenda ya michezo ya tenisi dunia.

Ushindi huo kwa Serena ni kama kulipiza kisasi dhidi ya Kelber kufuatia Mjerumani huyo kumshinda katika fainali ya michuano ya wazi ya Australia Iliyofanyika mapema mwaka huu mjini Melborne nchini Austalia.

Lakini pamoja na Serena Williams kufikia rekodi ya Gwiji wa Ujerumani Graf ya kuwa bingwa wa wakati wote wa michuano ya ubingwa mkubwa ama michuano mikubwa ya tenisi ya Grand Slam kwa mtu mmoja mmoja [singles], bado mchezaji huyo anakuwa nyuma mara mbili kwa mchezaji kiongozi wa muda wote wakutwaa mataji makubwa Margaret Court, ambapo raia huyo wa Australia yeye alishinda mataji 13 kati ya 24 katika michuano hiyo mikubwa wakati huo ikiwa ya ridhaa kabla ya baadaye kubadilika na kuwa ya kulipwa mnamo mwaka 1968.

Fainali nyingine ya mtu mmoja mmoja kwa upande wa wanaume itamkutanisha mwenyeji wa michuano hiyo Mwingereza Andy Murray ambaye ni mchezaji bora namba moja kwa sasa nchini Uingereza kwa upande wa wanaume akicheza fainali ya tatu ya michuano hiyo ambapo yeye atakuwa katika kibarua dhidi ya mchezaji Milos Raonic siku ya jumapili Julai 10 mwaka huu.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya