Jumanne , 6th Aug , 2019

Mwanamichezo wa mpira wa kikapu nchini Marekani Donell Cooper, amezua gumzo ulimwenguni baada ya kupimwa mkojo na kukutwa mjamizito wakati anafanya vipimo vya afya ili kujiunga na timu nchini Bosnia Herzogovina.

Mwanamichezo wa mpira wa kikapu nchini Marekani Donell Cooper

Inadaiwa kuwa mchezaji huyo ametumia mkojo wa mpenzi wake ili kukwepa kupimwa kwa sababu alikuwa anatumiwa dawa za kuongeza nguvu.

Kipimo cha kumgundua mtu anayetumia madawa ya kulevya kiitwacho Human Chorionic Gonadotropin (HGO) kimeonyesha kuwa mchezaji huyo ni mjamzito.

Baada ya kugundulika kuwa ametumia mkojo wa mpenzi wake Donell Cooper amesema hata yeye alikuwa hajui kama mpenzi wake ni mjamzito na amefanya hivyo ili kukwepa kugundulika kama anatumia dawa ya kuongeza nguvu.

Mchezaji huyo wa zamani wa timu ya Monaco na Ohio kwa sasa amefungiwa miaka 2 na chama cha mpira wa kikapu duniani (FIBA) kutojiuhusisha na mchezo huo.