Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

MVP wa Sprite Bball Kings, aweka rekodi Taifa Cup

Ijumaa , 21st Dec , 2018

MVP wa michuano ya Sprite Bball Kings mwaka 2018, Baraka Sadick ameendelea kuonesha ubora wake baada ya kuweka rekodi ya kufunga pointi 72 katika mchezo mmoja kitu ambacho hakijawahi kutokea katika historia ya mchezo wa kikapu nchini.

Timu ya Mchenga Bball Stars walipokabidhiwa kombe pamoja na tuzo ya MVP.

Baraka ambaye alikuwa anachezea timu ya mabingwa wa Sprite Bball Kings, Mchenga Bball Kings ameweka rekodi hiyo Katika mashindano ya Taifa Cup yanaoendelea mkoani Simiyu ambayo yamefikia hatua ya fainali na inapigwa kesho ikikutanisha timu anayochezea Baraka ya mkoani wa Dar es Salaam (Dream team) dhidi ya timu ya mkoa wa Mwanza.

Katika mchezo wa nusu fainali dhidi ya timu ya mkoa wa Mara, Baraka alifunga pointi 72 ndani yake akifunga 'Three point' 17 na kufanya mpaka sasa kwa Tanzania yeye ndio aliyefunga Three points nyingi kuliko mchezaji yeyote.

Pia katika michezo mingine, Baraka amekuwa akiongoza kwa kufunga pointi nyingi hivyo kuendelea kuwa miongoni mwa wachezaji bora zaidi wa Kikapu kuwahi kutokea.

Katika mechi dhidi ya Mwanza alifunga pointi 38, Rebound 2 na Assists 3 huku Three pointi zikiwa 3. Dar es salaam iliibuka na ushindi wa pointi 95 kwa 45 za Mwanza.

Mchezaji Baraka Sadick akikimbia na mpira kwenye game 1.ya fainali dhidi ya Flying Dribblers

Katika mechi nyingine dhidi ya Singida, Baraka alifunga pointi 56, Rebound 4 na Assists 9 na Three pointi zilikuwa 11. Dar es salaam ilishinda kwa pointi 171 kwa 29 za Singida.

Kwenye mechi dhidi ya Shinyanga, Baraka alifunga pointi 26, Rebound 1, Assists 3, huku akifunga Three pointi 6, Dar es salaam ikishinda pointi 107 dhidi ya 70 za Shinyanga.

Kabla ya fainali ya kesho itakayopigwa saa 10:00 jioni, Baraka ana wastani yaani 'Avarage' ya pointi 48 kwa kila mchezo na Assists 7 kwa kila game, pia Rebound 2 kwa kila mchezo.
 

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya