
Mohammed Dewji
Mo Dewji ametoa malalamiko hayo kupitia kurasa zake za mkitandao ya kijamii, akitolea mfano goli la Luis Miquissone dhidi ya Mwadui FC, lililokataliwa kuwa ni la kuotea.
Bado dhulma juu yetu inaendelea. Kwa mwenendo huu, mpira wetu hapa Tanzania kamwe hauwezi kusonga mbele. pic.twitter.com/lAo4iDuvf9
— Mohammed Dewji MO (@moodewji) November 1, 2020
Waamuzi wa Tanzania wamekuwa wakilalamikiwa juu ya uchezaji wao hususani kwenye maamuzi yenye utata kama ya kuotea na matukio ya katikati ya uwanja.
Hivi karibuni Shirikisho la soka Tanzania kupitia Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu soka Tanzania bara ilimfungia mwamuzi Shomari Lawi miezi 12 kutojihusisha na soka kutokana na makosa mbalimbali katika kazi yake.