Jumamosi , 15th Mar , 2014

Kuwasili kwa mikanda hiyo PST yasema ni makamilisho ya maandalizi

Shirikisho la ngumi za kulipwa Tanzania PST hii leo limepokea mikanda miwili ya ubingwa wa kimataifa na wa dunia kwa bara la afrika iliyoagizwa toka nchini Denmark

Katibu mkuu wa PST Anthony Rutta amesema kuwa kuwasili kwa miakanda hiyo miwili ni kiashirio cha kukamilika kwa maandalizi ya mapambano makubwa mawili yatakayopigwa march 29 mwaka huu katika ukumbi wa PTA jijini Dar es salaam
Ambapo mpambano mkubwa main card ni kati ya mabondia Thomas Mashali atakayevaana na Japhet Kaseba

Rutta amesema tayari kwa asilimia 95 kila kitu kimekamilika kwa mapambano hayo na hivyo kuwataka mabondia wote watakaopanda ulingoni siku hiyo waendelee na maandalizi mazito na kujipanga kutoa burudani kwa mashabiki watakaofika kutazama mapambano yote siku hiyo.