Jumanne , 1st Apr , 2014

Chama cha mchezo wa JUDO Tanzania bara JATA kimesema kuwa wamemaliza mvutano uliojitokeza dhidi ya wenzao wa Zanzibar baada ya kufanya kikao nakukubaliana namna ya kuwapata wawakilishi watakaowakilisha Tanzania.

Wawakilishi hao wataenda kuiwakilisha Tanzania, katika michuano ya jumuiya ya madola itakayofanyika jijini Grascow Scotland.

Katibu mkuu wa JATA Innocent Malya, amesema kuwa baada ya maafikiano sasa kila kitu kiko sawa na wamekubaliana watumie mashindano ya Afrika Mashariki kupata wawakilishi wa pande zote, kwa sifa ile ile ya mshindi wa medali ya dhahabu ndiye atakayefuzu kuwakilisha nchi katika michuano hiyo.