
Kabange amesema, wanajaribu kutafuta mechi za kirafiki za nguvu ili ziweze kuwasaidia kuimarisha kabisa kikosi chake.
Kabange amesema, "Unapopata mechi za kirafiki zinakupa mwelekeo kama kikosi chako kipo tayari au bado na zinakusaidia kuweza kutambua ni kitu gani unatakiwa kuongeza au kuboresha katika kikosi chako".
Kabange amesema, kwa sasa anawajenga mwili wachezaji wake ili kuwa katika hali nzuri ya kimchezo na kuweza kufanya vizuri ili kutoka katika nafasi waliyopo hivi sasa.